Friday, 16 August 2013

BARNABA AIKOSA FIESTA YA KIGOMA

MKALI wa songi la ‘Sorry’,  Barnabas Elias ‘Barnaba Boy’, ameikosa Fiesta ya Kigoma kutokana na tarehe hiyo kuingiliana na arobaini ya mama yake mzazi aliyefariki siku za hivi karibuni.
Akizungumzia ishu iyo jana katika klabu ya Jacaranda iliyopo Kinondoni jijini Dar, Barnaba alisema hakwenda Kigoma ili amalizie arobabini ya mama yake.
“Siku ya Fiesta Kigoma ndiyo siku ya arobaini ya mama yangu na ndiyo maana unaniona niko hapa sijaenda Kigoma,” alisema Barnaba.
Uzinduzi wa tamasha hilo la Fiesta unatarajiwa kufanyika Jumamosi ya Agosti 17, mwaka huu mkoani Kigoma.

No comments:

Post a Comment