Showing posts with label Lad jay dee. Show all posts
Showing posts with label Lad jay dee. Show all posts

Monday, 16 September 2013

KIATU CHA THAMANI CHAMUANGUSHA LADY JAY GEE JUKWAANI NA KUTEGUKA MGUU

 
                Lady Jaydee akiwa backstage na kiatu chake kilichosabisha ateleze jukwaani
Katika show hiyo Lady Jaydee alinunua kiatu cha rangi ya blue, kirefu aka high heels chenye thamani ya shilingi 168,000. Yes laki moja na elfu sitini na nane kama masikio yetu hayakutudanganya.
Hata hivyo urefu wa kiatu hicho ameutaja kuwa chanzo cha kuteleteza jukwaani kwenye show hiyo na kukaribia kumwangusha.
“Kuanguka jukwaani ni ajali kama ajali zingine, isitoshe sikuanguka bali nilikaribia. Ila poleni kwa mlioumizwa na hicho kitendo…Nitapunguza urefu wa viatu siku nyingine,” aliandika jana kwenye ukurasa wake wa Facebook.
“Ni bahati mbaya tu, kwani hata Mwanza/Kahama/Dodoma vilikuwa virefu kama hivyo hivyo na sikuteguka,” alitweet kufafanua kuhusu uvaaji wa viatu virefu jukwaani

Wednesday, 11 September 2013

MASTAA WA BONGO WALIONASA MIMBA NA KUCHOROPOKA BILA SABABU KUWEKWA WAZI

             DHAMIRA ya watu wengi ni kutunza mimba hadi kufikia hatua ya kujifungua lakini wakati mwingine ujauzito unaweza kuchoropoka kutokana na sababu tofauti, iwe kwa kukusudia au bahati mbaya.Kwenye maisha ya mastaa wetu wa Bongo, wapo waliowahi kupata mimba lakini kutokana na sababu tofauti, zilichoropoka.
Amani linakumegea baadhi ya mastaa hao ambao wengine walianika sababu za mimba hizo kuchoropoka huku wengine wakifanya siri:


http://lh6.ggpht.com/_1F5PLxca91g/S1woZhVXMjI/AAAAAAAADmM/D1lQ2ywdEE8/aunti%20ezekiel1.jpg
            AUNT EZEKIEL
Februari, 2011 aliripotiwa kuwa na ujuzito wa mwanaume ambaye mwenyewe hakumtaja lakini haikupita muda mrefu, mimba hiyo ilichoropoka pasipo kuweka wazi sababu.
http://api.ning.com/files/Dz3XGZp1879BBftYCfjCc*FHY0JOLwj9ZCs9mYAg*6QiA2pMaoHtFj4Cge75oreNDd9cs*02GOhuovuY*tFfhgGosZ3*XK8e/jinikabula.jpg?width=550
     JINI KABULA

Mwaka jana alijinadi kuwa na ujauzito wa Mbongo Fleva, Maximiliam Bushoke. Mimba hiyo ikadumu kwa miezi kadhaa, ghafla ikachoropoka yenyewe kwa bahati mbaya.
http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2012/10/Wema.jpg
WEMA SEPETU

Kwa upande wake alitundikwa kibendi na aliyekuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’ lakini miezi kadhaa mbele ikatoka yenyewe kutokana na sababu za kitaalam.
http://api.ning.com/files/aoTSsYzQOjApgrpXrEY96gE0HbMxZ8tdB8x80IZJMWGB6rbIdkcEWpWRVrCjRG7J0RxADcxKZLxX1kQFGkU3lTO1AnFGzFpO/206668_178597685521700_100001144098952_370032_2266125_n.jpg?width=398&height=600
LULU
Mwaka jana aliripoti kwenye vyombo vya habari kuwa na mimba ya muigizaji mwenzake, marehemu Steven Kanumba. Wakati mapaparazi wakiendelea kufanya uchunguzi, ghafla ikadaiwa ‘kuyeyuka’ pasipo kujulikana chanzo.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiExW1RPFRvAXG9V421aV5z2gBMr3KZSnCC1BEw0vYQrtB1bvRaWO1UT4BEPh2KtwqX4t1iKtIKBwmNQ5rCT6bGwAkfd_0z-Nqlu9wp1Y6UJ3P-wgfoS-kqqE_3KWoo1MsYtgWT1JMdMFU/s640/jay+dee.jpg
LADY JAYDEE
Huyu ni mke halali wa Mtangazaji, Gardner Habash. Mwaka 2011 mitandao ya kijamii iliripoti kuwa ni mjamzito na kudaiwa kuwa habari hiyo ilimpa faraja mumewe lakini furaha hiyo iliyeyuka ghafla wakati Lady Jaydee akionekana na tumbo kubwa, ikadaiwa mimba imechoropoka bila sababu kutajwa.

Baby Madaha

Mwaka 2010 mkali huyo wa filamu na muziki Bongo, alidaiwa kuwa na mimba ingawa mwenyewe hakutaka kuweka wazi lakini baadaye ilidaiwa kuwa alikwenda kuichoropoa nchini Kenya.
http://www.gushit.com/files/bookmark_photos/a7468b0461L.jpg
JACK WA CHUZ

Mapema mwaka huu aliripotiwa kuwa ni mjamzito lakini mwenyewe hakupenda kuweka mambo yake hadharani. Hata hivyo, vyanzo makini vilidai kuwa mimba hiyo ilikuwa ya mfanyabiashara mmoja jijini Dar lakini baadaye aliichoropoa pasipo kufahamika sababu
-USWAZI

Monday, 2 September 2013

LADY JAYDEE, AFANDE SELE, MKOLONI NA JB WAKIMBILIA CHADEMA



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeendelea kuwavuta wasanii kujiunga na chama hicho, ambapo sasa wasanii wanne wa muziki wa kizazi kipya, maarufu Bongofleva na filamu, wanatarajiwa kutangazwa kuhamia chama hicho wiki hii. 


Wasanii hao wanadaiwa tayari kukubali kuingia kwenye chama hicho na wanatarajiwa kutangazwa rasmi hadharani katika mkutano wa hadhara utakaofanyika jijini Dar es Salaam.
 
Kukubali kwao kuingia katika siasa, kunatajwa kutokana na ushawishi mkubwa uliofanywa na wabunge vijana wa chama hicho, pamoja na Diwani wa CCM kutoka kata moja ya Wilaya ya Kinondoni, ili chama hicho kivune kura za vijana katika uchaguzi mkuu wa 2015.
 
Wabunge hao wa Chadema na majimbo yao katika mabano ni Halima Mdee (Kawe); Kabwe Zitto (Kigoma Kaskazini); John Mnyika (Ubungo) na Joseph Mbilinyi, jina la kisanii Sugu (Mbeya Mjini).
 
Habari kutoka kwa watu wa karibu na wasanii hao pamoja na ndani ya Chadema, zinawataja wasanii hao kuwa ni wanamuziki Judith Wambura maarufu Lady Jaydee na wa miondoko ya Hip hop, Selemani Msindi ama Afande Sele.
Taarifa zinawataja wengine kuwa ni mwanamuziki Fredy Maliki maarufu Mkoloni na mwigizaji wa filamu, Jacob Steven kwa jina la kisanii JB.
 
Inadaiwa wasanii hao lengo la kuingia katika siasa kupitia chama hicho, ni kuwania ubunge ambapo Jaydee anatajwa kutaka kugombea wilayani Musoma; Afande Sele Morogoro Mjini; Mkoloni Jimbo la Tanga na JB Jimbo la Mkoa wa Dar es Salaam.
 
Hata hivyo gazeti hili lilipowatafuta kuzungumzia taarifa hizo wote walikana ingawa wapo waliokiri kushawishiwa kuingia kwenye chama hicho na viongozi wa Chadema na wananchi, ili wagombee ubunge.
 
 Afande Sele alikana kujiunga na chama hicho na kusema hana taarifa hizo isipokuwa ni kweli ameshawahi kufuatwa na viongozi wa Chadema wa Mkoa wa Morogoro, wakimtaka ajiunge na chama hicho na agombee ubunge Morogoro Mjini.
 
“Nimeshafuatwa na viongozi wa Chadema wa mkoa na kata nijiunge na chama hicho na nigombee ubunge …tena hata vijana wengi na baadhi ya wazee wamenitaka nigombee ubunge kwa kupitia Chadema lakini nimekataa.
 
“Pia Sugu ni mshikaji wangu na anapokuja Morogoro, vijiwe vyake ndio vyangu naye vijana wameshamfuata wakimwambia anishawishi nigombee ubunge kupitia Chadema, amekuwa akiniambia vijana wananitaka lakini mimi sitaki, sijawahi kujiunga na chama chochote na naona mbunge wa sasa (Abdulaziz Aboud) anafanya kazi nzuri.
 
“Mimi sio mwanasiasa, lakini ni mwanaharakati kupitia muziki na mtandaoni na nimekuwa nikitoa maoni mengi na kukosoa lakini narudia si mwanasiasa na sijawahi kujiunga na chama chochote,” alisema Afande Sele.
 
Vilevile amekanusha kushawishiwa na viongozi wa kitaifa wa Chadema au wabunge, ingawa amekiri kuna wabunge wa chama hicho kuwa ni marafiki zake wakiwemo Mbilinyi na Zitto.
 
Kwa upande wa Jaydee alisema hafuati itikadi ya chama chochote cha siasa na hapendi siasa kutokana na imani kuwa siasa ni uongo na yeye hapendi uongo. Alisema hana nia ya kujiunga na chama chochote cha siasa wala kugombea ubunge kupitia chama chochote.
 
Hata hivyo alipoulizwa iwapo atagombea baada ya Katiba kuruhusu mgombea binafsi, alisema kwa wakati huo atajua.
Hata hivyo, Licha ya kuwaona wanasiasa ni waongo, anakiri wapo wanasiasa anawaamini kutokana na kazi zao na kumtaja miongoni mwao ni Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo na Mbunge wa Afrika Mashariki, Shy-rose Bhanji.
 
Mwanamuziki huyo alisema licha ya kuwa na marafiki wa Chadema na CCM kama Sugu na Profesa Jay wa Chadema na Mbunge wa Viti Maalumu, Catherine Magige na Bhanji wa CCM, hawajawahi kumshawishi kujiunga na vyama vyao. 
 
Mkoloni Akizungumzia taarifa hizo za kujiunga na Chadema, JB alikana na kusema; “mimi na siasa ni vitu tofauti, sijawahi kufuatwa na mtu wa Chadema na angalau kungekuwa na dalili basi uniulize, hiyo ni taarifa ya kutengenezwa na wewe ndiye uliyetengeneza hakuna aliyekupa ni udaku huo.”
 
Kwa upande wa Mkoloni, alisema hajawahi kufuatwa wala kushawishiwa kujiunga na chama chochote, isipokuwa ni mwanachama wa muda mrefu wa Chadema na amekuwa akishiriki kampeni, mikutano ya hadhara na matukio yote ya uhamasishaji ndani ya chama hicho. 


Alisema kuhusu kuombwa kuwania jimbo mkoani Tanga kwa tiketi ya chama hicho, alisema hajawahi kuombwa na chama hicho kufanya hivyo.
 
“Sijawahi kuombwa nigombee jimbo, na kuhusu nia ya kugombea, ni mapema mno kuzungumzia suala hilo sasa na hata kanuni za chama changu haziruhusu labda uniulize swali hilo mwakani naweza kuwa na jibu,” alisema Mkoloni.
 
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, alikataa kuzungumzia taarifa hizo akidai yuko barabarani na masuala yote yanayohusu chama hicho aulizwe Msemaji wa chama hicho.
 
Hata hivyo msemaji wa chama hicho, Tumaini Makene alisema hana taarifa kuhusu kufanyika kwa mkutano wa chama hicho Dar es Salaam na kutaka apewe muda afuatilie taarifa hizo.

-Habari leo

Saturday, 17 August 2013

FEZA KESSY NI MIONGONI MWA WASANII WALIOKUWA WAMEVAA VIBAYA KATIKA UZINDUZI WA VIDEO YA YAHAYA YA LADY JAYDEE

 Video ya yahala ilizinduliwa rasmi jana pande za nyumbani lounge. Baadhi ya wasanii kama Feza Kessy ambaye alikuwa mgeni rasmi, Vanessa Mdee  na  Mkolon...

Pamoja  na  kuwa  mgeni  rasmi, Feza  anadaiwa  kuwa  miongoni  mwa  wasanii  waliokuwa  wamevaa  vibaya....

Vazi   lake  lilikuwa  likiyaanika  matiti  yake  hadharani, hali  ambayo  iliwafanya  hata  watoto  wayashuhudie. 










ANGALIA VIDEO YA WIMBO MPYA WA LADY JAY DEE-YAHAYA