Showing posts with label Linah. Show all posts
Showing posts with label Linah. Show all posts

Thursday, 19 September 2013

VIDEO:LINAH AKIFUNGUKA JUU YA PENZI LAKE NA AMINI


Msanii wa muziki wa bongo fleva ambaye sasa ni mjasiriamali pia Anasteria Sanga Linah au muite Ndege Mnana amefunguka kuwa producer wa studio ya Bhitz Pancho Latino ndiye mwenye siri nzito ya penzi lake na msanii mwenzake Amini ambaye kwasasa penzi lao limekuwa stori ya kale baada ya kuachana.
Linah amesema tokea wanaanza mapenzi yao Pancho ndiye alikuwa mtu pekee anayejua mambo mengi kuwahusu wao na jinsi walivyotumbukia katika penzi ambalo anasema yeye binafsi ndiye hasa alikuwa akimpenda Amini kupita kiasi japo baadaye akagundua kuwa hata mwenzake naye anamzimika na hivyo penzi likawa linasonga.

"Yaani we muulize Pancho yule ndio ana siri kubwa sana ya penzi langu na Amini,yaani jamani nilimpenda sana Amini mpaka nikakubali kuingia kwenye mapenzi na nilimpenda hasa kutoka moyoni,kuna vitu vingi nyuma yake ambavyo Pancho anajua",alisema Linah.

Msanii huyo mwenye sauti tamu kiasi cha kupachikwa jina la Ndege Mnana na msanii mkongwe Patricia Hillary ameendelea kufunguka kuwa wakati ameangukia katika penzi la Amini alikuwa anawachomolea wanaume wengi waliokuwa wanamtokea tena wenye pesa zao na wengine ni watu wazito lakini aliamua kutoka moyoni kwa dhati kuwa na Amini kwahiyo akawa anamtunzia heshima yake.

Anasema kama angekuwa macho juu kuna uwezekano mkubwa asingeendelea kuwa na Amini au angekuwa anamsaliti kwa kiasi kikubwa lakini moyo wake usio na tamaa ndio ulikuwa unamfanya aendelee kumpatia penzi la kweli.

Akavujisha siri kuwa Amini ndiye aliyemtibua na ndipo akapitisha uamuzi wa kujiweka pembeni kwasababu ambazo ni ngumu kuziweka hadharani lakini mpenzi wake huyo wa zamani anazijua na ni sababu ambazo haziwezi tena kulirudisha penzi lao japo anakiri kuwa aligundua kuwa mpenzi wake huyo wa zamani anampenda siku alipomtamkia kuwa mapenzi yameisha kila mmoja ashike lake.

Anasema katika kuonesha kuwa ameachana na Amini lakini hana bifu naye wakaamua kutoa wimbo wa pamoja wa Mtima wange.

Akizungumzia show anazofanya na Amini jukwaani wakiwa kama wapenzi anasema ni kuonesha kuwa hakuna bifu na hata mabusu anayopigwa na zilipendwa wake huyo anayapokea kwasababu anashindwa kuyapotezea jukwaani akiogopa kumtia aibu jamaa huyo mbele ya mashabiki na watu wengine.

Cheki video ya vitu vingine alivyofunguka katika interview niliofanya nae katika kipindi cha Hatua Tatu cha Times fm.

Friday, 30 August 2013

DIAMOND, LINAH NDANI YA PENZI JIPYA?CHEKI MAMBO YAO...!!

              Tabia mbaya! Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amenaswa na msanii mwenzake, Esterlina Sanga ‘Linah’ wakiwa kwenye mapozi ya kimahaba ambayo yametafsiriwa vibaya.
 Katika tukio hilo lililojiri juzikati kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora ndani ya Tamasha la Serengeti Fiesta, Diamond alishuhudiwa akiwa amempakata Linah ndani ya basi huku mikono ya jamaa huyo ikishika maeneo nyeti.
Mara baada ya kutimba uwanjani hapo wakitokea hotelini tayari kwa kufanya shoo, Diamond na Linah walibaki kwenye basi wakiwa wamepakatana na hata msichana huyo alipomaliza shoo yake kali mishale ya saa 3: 00 usiku, alirejea mikononi mwa Diamond ambaye alimpachika mapajani.
 Shushushu wetu aliwapiga chabo ‘wakifanya yao’ hadi Diamond alipokwenda stejini na kuangusha bonge la shoo huku akimwacha Linah mpweke.
Kwa mujibu wa mashuhuda, kama kweli mchumba wa Diamond, Penniel Mungwilwa ‘Penny’ anakubali mambo kama hayo, basi atakuwa na roho ngumu au moyo wa chuma.