Showing posts with label LULU. Show all posts
Showing posts with label LULU. Show all posts

Thursday, 19 September 2013

LULU AMPONZA RICHIE!


             KUFUATIA kitendo cha galacha wa sinema za nyumbani, Single Mtambalike ‘Richie’ kumtunza fedha nyingi msanii mwenzake Elizabeth Michael ‘Lulu’ hivi karibuni, warembo wengi wa mjini wamekuwa wakimsumbua wakitaka kuzichuma.
Akizungumza na paparazi wetu Jumanne ya wiki iliyopita, Kinondoni Makaburini, jijini Dar, Richie alikiri kupokea simu nyingi za kina dada tangu siku ile ya uzinduzi wa filamu ya Lulu, Foolish Age uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City wakimuomba urafiki wa kawaida kumbe wana yao moyoni.
“Duh! Umeipata! Ni kweli kabisa simu ni nyingi siku ile tulikutana na mashabiki wetu wengi sana, wakachukua namba lakini kumbe wengi wao lengo lilikuwa ni kutaka mkwanja, daah Napata usumbufu kweli kwa kupigiwa simu kila dakika,” alisema Richie.

Thursday, 12 September 2013

BAADA YA UZINDUZI WA FILAMU YA LULU "FOOLISH AGE"...!! SASA LULU AANZA KUPOKEA VITISHO

 
KUFANIKIWA kwa uzinduzi wa filamu ya Foolish Age ya msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’ uliofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, kumemfanya kinda huyo anayetingisha katika tasnia hiyo kupata vitisho kutoka kwa mastaa wenzake.

Habari kutoka vyanzo mbalimbali ndani ya fani hiyo zinasema katika uzinduzi huo, msanii huyo alifunika na kuonyesha dalili zote za kuwazima mastaa wenzake ambao kwa muda mrefu wamekuwa juu.
Taarifa hizo zinasema staa huyo wa Bongo Muvi anatafutwa kwa kila namna, usiku na mchana ili kuhakikisha nyota yake inafifia.
Madai hayo yamekuja zaidi baada ya uzinduzi huo kufana kwani pamoja na mambo mengine, hata jinsi alivyokuwa amejipanga kwa walinzi wake, lilikuwa ni jambo kubwa ambalo linafanana na inavyotokea katika shughuli za mastaa mbalimbali wa majuu.
Mwandishi wa gazeti hili aliamua kufunga safari hadi maskani kwao pande za Tegeta, lakini msanii huyo hakupenda paparazi afike kwao hivyo mazungumzo yao kufanyika kama ifuatavyo kwa njia ya simu ya kiganjani.
Mwandishi: Mambo vipi Lulu?
Lulu: Salama tuu za kwako?
Mwandishi: Salama, vipi umesikia vitisho vyako kutoka kwa mastaa wa Bongo Muvi wanaodai kuwa umekuja kuwapita kisanii?
Lulu: Hapana sijasiki, lakini kama wanatoa vitisho lazima wakubaliane na ukweli kwamba lazima awepo wa kwanza na wa mwisho, wakaze buti.
Mwandishi: Umejipangaje kukabiliana na hilo?
Lulu: Najipanga kufanya kazi mimi kama mimi na wao wafanye kama wao, wakijifanya kuwa kama mimi haiwezi kuwa hivyo, mbona mastaa wa ughaibuni kama Beyonce na Rihanna wako tofauti? Lazima awepo wa kwanza mpaka wa 10 hatuwezi kulingana.
Mwandishi: Kuna lolote la kuongeza juu ya hilo ama wito kwa wasanii?
Lulu: Wajipange kufanya kazi kwa nguvu zote, wasifanye kama mimi wafanye kama wao,
Mwandishi: Asante Lulu nakutakia siku njema
Lulu: Ok, sawa kazi njema

SOURCE: GPL

Tuesday, 10 September 2013

LULU ATEULIWA KUWA BALOZI WA DAR FILAMU FESTIVAL..!!

            Ikiwa ni wiki moja imepita toka mwigizaji mrembo wa Bongo Movie Elizabeth Michael aka Lulu azindue filamu yake ya ‘Foolish Age’ katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es salaam milango yake ya mafanikio imeendelea kufunguka.
lulu4


Dar Filamu Festival Idara Habari Maelezo jana
Kupitia akaunti yake ya Instagram @Hotlulumichael, ameweka picha akiwa na waandaaji na kutoa shkurani zake kwa kuchaguliwa kuwa Balozi wa ‘Dar Filamu Festival’. 
“Shukrani za dhati kwenu DAR FILAMU FESTIVAL kwa kunichagua kuwa BALOZI wenu(OFFICIAL ACTRESS 2013/2014)…”

Lulu kwa sasa anafanya shughuli zake za filamu chini ya kampuni ya Proin Promotions.
Dar Filamu Festival (DFF) ni tamasha la filamu linalotarajiwa kufayika kwa siku tatu kuanzia (September 24-26) katika viwanja vya posta-Kijitonyama, Dar es salaam. Kwa mujibu wa filamucentral, tamasha hilo litaambatana na utoaji wa Semina kwa wadau wa filamu, kuonesha filamu za kitanzania kwa watu wote bure na kutakua na filamu nne kwa siku kuanzia saa kumi na mbili jioni mpaka saa tano usiku.

Sunday, 1 September 2013

VIDEO: LULU AKIIMBA WIMBO WA YAHAYA WA LADY JAYDEE LIVE JUKWAANI KWENYE UZIDUZI WA FILAMU YAKE


Elizabeth Lulu Michael anaweza kuimba. Alithibitisha live jana kwenye uzinduzi wa filamu yake, Foolish Age, pale alipopanda kwenye stage na kuimba kwa ufasaha na Lady Jaydee hit yake Yahaya. Kutokana na kuimba kwa ustadi na bendi ya Machozi, Lulu alituzwa na mvua ya hela na mashabiki, Tazama video.

Saturday, 31 August 2013

PICHA:LULU AZINDUA RASMI FOOLISH AGE

 

 
 
 
 
 
MSANII wa Filamu Bongo, Elizabeth Michael 'Lulu', usiku wa kuamkia leo amefanikisha zoezi la uzinduzi wa filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Foolish Age .

 Baada ya move hiyo kali ya dakika 120 iliyooesha ukali wa staa huyo kuoneshwa kwa dakika 20 tu na kubakisha zingine 100 kusubiri wateja kuziona majumbani kwao alipanda jukwaani kujitambulisha na kutoa shukrani kwa wamepenzi wa tasnia ya filamu nchini Tanzania kwa muitikio wao alipanda na kuimba wimbo huo wa Yahaya.

Akianzia kuimba kiitikio cha wimbo huo akiwa Back Stage, Lulu aliwashangaza watu pale alipomudu vyema wimbo huo kiasi cha mashabiki ‘Mapedeshee’ wakiongozwa na Pedeshee Rich Rich, kupanda jukwaani na kumtunza fedha kibao ambazo hakika zilimpagawisha msanii huyo na mwisho wa wimbo huo alisema mziki unalipa.

Tukio la uzinduzi huo lilifanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar, na kuhudhuriwa na mastaa kibao wa tasnia mbalimbali hapa Bongo, wakiwemo; Judith Wambura 'Lady Jaydee', ambaye alitumbuiza sambamba na Barnaba na Amini.
 Wasanii mbalimbali walihudhuria show hiyo usiku huu pale Mlimani City

 Lulu akizungumza machache mara baada ya Move yake hiyo kuoneshwa kwa mashabiki na wapenzi wa filamu Tanzania ndani ya Ukumbi wa Mlimani City.

 Wadau walifuatilia burudani...
 Jide akikamua jukwaani...
 Mama na mwanao ni kama chanda na Pete... huyo ni Natasha (kulia) na Bintiye Monalisa.
 .... Walitunzana tu kivyao vyao...
 noti alizo tuzwa
 Rich Rich akimwaga noti
 Wadau wakifuatilia uzinduzi huo wa Filamu.
 Furaha ilitawala
 Mwogozaji wa Filamu za Kibongo, Leah Mwendamseke nae alikuwepo kuangalia kazi hiyo ya Lulu.
 Waongoza Shughuli hiyo watangazaji wa Redio na TV Double G na mwana dada kutoka Times FM walikuwepo.

LULU AJAZWA MAHELA MA MAPEDESHEE BAADA YA KUIMBA WIMBO YAHAYA WA LADY JAY DEE

UIMBAJI stadi wa Wimbo wa YAHAYA wa Nguli wa muziki wa Kizaki kipya Lady Jay Dee umemjaza mahela Msanii wa Filamu aliyejizolea umaarufu kwa miaka ya hivi karibuni, Elizabeth Michael ‘Lulu’ wakati akiimba wimbo huo na Jide wakati wa uzinduzi wa Video yake mpya na yakwanza kusimama peke yake ya FOOLISH AGE.
Baada ya move hiyo kali ya dakika 120 iliyooesha ukali wa staa huyo kuoneshwa kwa dakika 20 tu na kubakisha zingine 100 kusubiri wateja kuziona majumbani kwao alipanda jukwaani kujitambulisha na kutoa shukrani kwa wamepenzi wa tasnia ya filamu nchini Tanzania kwa muitikio wao alipanda na kuimba wimbo huo wa Yahaya.
Akianzia kuimba kiitikio cha wimbo huo akiwa Back Stage, Lulu aliwashangaza watu pale alipomudu vyema wimbo huo kiasi cha mashabiki ‘Mapedeshee’ wakiongozwa na Pedeshee Rich Rich, kupanda jukwaani na kumtunza fedha kibao ambazo hakika zilimpagawisha msanii huyo na mwisho wa wimbo huo alisema mziki unalipa.
“Jamanieee kumbe mziki unalipa ile mbaya yaani  nimeimba ubeti mmoja tu hapa ona hela kibao, kuanzia sasa na mimi nitaanza kuimba mziki”, alisikika Lulu akisenma huku akishangiliwa na mashabiki wake.

Sunday, 25 August 2013

HATIMAYE "FOOLISH AGE" YA LULU MICHAEL YARUHUSIWA BAADA YA KUZUIWA

Bodi  ya   ukaguzi  wa  filamu  Tanzania  imeridhia  na  kuiruhusu  filamu  ya  Foolish Age  ya  Lulu  Michael  iingie  sokoni  baada  ya  kuizuia  hapo  juzi....
Filam  hiyo  ilizuiliwa   kutokana  na  mavazi  ya  nusu  uchi  yaliyokuwa  yamevaliwa  na  washiriki  wake  na  kumtaka  Lulu  Michael  aifanyie  marekebisho  kwa  kuviondoa  vipande  hivyo  ambavyo  vilikuwa  kinyume  na  maadili  ya  kitanzani....
Filamu hiyo  ambayo yupo Lulu, Diana Kimaro, Jengua na Hashim Kambi itazinduliwa tarehe 30 mwezi huu katika ukumbi wa Mlimani City
Kupitia  account  yake  ya  instagram, Lulu  amepost  ujumbe  huu.

 

Friday, 23 August 2013

BODI YA UKAGUZI YAIPIGA STOP FILAMU YA "FOOLISH AGE" YA LULU...HII NDIO SABABU

Bodi ya ukaguzi wa filamu na michezo ya kuigiza nchini imeipiga stop filamu ya Foolish age ya msanii wa kike mwenye mvuto Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ baada ya kukuta picha zilizo nje ya maadili ya Kitanzania katika filamu hiyo, filamu hiyo ambayo ilipanga kuzinduliwa mwezi huu tarehe 30 katika ukumbi wa Mlimani City inahitaji marekebisho.


Kikwazo kilichoikumba filamu hiyo ni nguo fupi zilizotumika katika waigizaji walioshiriki katika filamu hiyo ambayo inatabiriwa kufanya vizuri katika soko la filamu Bongo kama itafanikiwa kuzinduliwa na kuingia sokoni, juhudi zinafanyika kuhakikisha kuwa marekebisho yanafanyika ili kwenda na ratiba kama ilivyopangwa.

Hivi sasa baada ya urasimishaji wa filamu mamlaka na taasisi zinazohusika na masuala ya filamu zimekuwa makini na kuhakikisha kuwa filamu zinazoingia sokoni na zile zinazozinduliwa kukaguliwa kabla ya kufanyika kwa matukio hayo kama ilivyokuwa awali, kama filamu hiyo ya Foolish age itashindwa vigezo vya madaraja yanayotolewa na Bodi hiyo haitaonyeshwa.

Lulu ndio mwigizaji bora wa kike kwa mwaka 2013 kupitia tamasha la filamu la kimataifa la ZIFF katika kipengere cha tuzo za Bongo movie kilichopewa jina la Zuku Bongo movie Awards zilizotolewa katika ukumbi wa Ngome Kongwe.


Friday, 16 August 2013

FOOLISH AGE’ YA LULU KUZINDULIWA AGOSTI 30

STAA  katika tasnia ya filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’,  anatarajia kuzindua filamu yake aliyoipa jina la Foolish Age Agosti 30, mwaka huu.



 Akiteta  na mtandao huu  hivi karibuni Lulu alisema  filamu hiyo ndiyo itakuwa ya kwanza  kuitoa tangu apate dhamana kutoka ‘lupango’ kuhusiana na kesi ya mauaji ya Kanumba.  Kwa mujibu wake, ndani ya filamu hiyo kuna vitu kavicheza ambavyo yeye mwenyewe alikuwa akivifanya enzi ya umri wake mdogo.
“Ni filamu yangu ya kwanza ambayo naamini mashabiki wangu wataipenda na licha ya wao kuipenda pia naamini watakaoiona watajifunza mengi sana,” alisema.
Uzinduzi wa filamu hiyo utafanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar, ukisindikizwa na Machozi Band inayoongozwa na Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’.

Thursday, 15 August 2013

HATIMAYE LULU AREJEA KUNDINI,ATAZINDUA MOVIE YAKE YA KWANZA TANGU ATOKE JELA,TAREHE 30 AUGUST

Muigizaji Elizabeth Michael (LULU) anatarajia kuachia movie yake ya kwanza tangu alipotoka jela "Foolsh Age" siku ya tarehe 30 mwezi wa nane katika ukumbi wa Mlimani City huku kukiwa na wasanii wa muzini pamoja na Jay Dee na Machozi Band ambao watasindikiza uzinduzi huo.
hotlulumichaelNina kila sababu ya kumshukuru Mungu....!!!ninafuraha ya kuwafahamisha kuwa TAREHE 30/8/2013 ndio siku nitakayozindua movie ya mpya ya FOOLISH AGE....hatimaye narudi kazini!!!!Uzinduzi utafanyika katika ukimbi wa MLIMANI CITY....kutakuwepo na wasanii mbalimbali wa muziki....na pia LADY JAY DEE pamoja na MACHOZI BAND atakuwepo pia!!!nahitaji support ya mashabiki wote wa LULU na mashabiki wa BONGO MOVIE.....♥♥♥♥!!!#PROINPROMOTERS