Showing posts with label BUNGENI. Show all posts
Showing posts with label BUNGENI. Show all posts

Monday, 16 September 2013

SUGU:"NDUNGAI ALIAMURU ASKARI WANIPIGE BUNGENI..."




            NI kauli iliyotolewa na Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’  Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amesema tukio la kupigwa ngumi na askari ndani ya Ukumbi wa Bunge lilisababishwa na  amri ya Naibu Spika, Job Ndugai na wala siyo askari.

Aidha Sugu alisema ilikuwa vigumu kuvumilia konde alilopigwa na askari wakati akitolewa nje kwenye vurugu zilizotokea bungeni hivi karibuni, ndiyo maana aliamua kulipiza kisasi kwa kutaka kumpiga ngumi na si kichwa kama anavyodai  askari.

‘Sugu’ alitoa kauli hiyo  wakati akiwahutubia wakazi wa Chunya Mjini kwenye mkutano wa hadhara ulioongozwa na Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, Dk Willibrod Slaa ambapo viongozi hao wapo ziarani  mkoani Mbeya  wakifanya  mikutano na wananchi kwa lengo la kuwaeleza ukweli wa kilichomtokea Sugu na  wabunge wengine bungeni hivi karibuni.

‘ Sugu’ alidai kuwa Ndugai ni adui wa wapinzani bungeni na kwamba kwa vyovyote vile ilikuwa vigumu kuvumilia kwa mtu yeyote baada ya askari kuanza kupiga wabunge kutokana na amri ya  Ndugai.

Naye Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Slaa akizungumzia suala hilo alisema kitendo alichofanyiwa Sugu hakikuwa kibaya kwake peke yake, bali hata wananchi waliomchagua.

Hata hivyo, Dk Slaa  alisema kwa upande mwingine ili heshima ya Bunge lolote lile duniani  iwepo, ni lazima wabunge watandikane makonde ndani ya Bunge  na si vinginevyo hivyo hashangai kwa kilichotokea kwa Sugu bungeni.

Dk Slaa, alimjia juu Ndugai akisema alikiuka Kanuni za Bunge kwa kitendo hicho na  kubainisha kwamba kanuni za Bunge zipo wazi kabisa  kwamba iwapo itatokea vurugu ndani ya Bunge anachotakiwa kukifanya ni kuahirisha Bunge kwa wakati huo.

Pia alisema askari ambao ni  wapambe wa Bunge ‘Sargent at arms’ ndio wenye mamlaka ya kuingia ukumbini na endapo itatokea nguvu ya ziada hao ndio wanaotakiwa kisheria na siyo kuwaita askari wa nje ya Bunge kuingia ndani.

Dk Slaa alisema kitendo kilichofanywa na Sugu pamoja na wabunge wengine ni cha kijasiri na aliwataka kutokurudi nyuma na misimamo yao  bali waendelee kusonga mbele.

Friday, 13 September 2013

TUNDU LISU AKAZA,AKATAA UAMUZI WA CCM KUTAKA KUIFUTA KESI YAKE



WAKATI viongozi mbalimbali wa CHADEMA wakiwasili mjini Dodoma kuungana na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, katika rufaa ya kupinga ubunge wake inayoanza kusikilizwa leo, mbunge huyo amekataa uamuzi CCM kutaka kuifuta kesi hiyo.

Juzi CCM kupitia kwa wakili wake, Godfrey Wasonga, iliwasilisha barua katika Mahakama ya Rufaa Dodoma na nakala kwa Lissu ikiomba mahakama hiyo kuifuta kesi hiyo.
 
  Kwa mujibu wa wakili huyo, sababu ya kuomba kufutwa kwa kesi hiyo ni walalamikaji wote kujitoa na kuapa mahakamani kuwa hawakuwa tayari kuendelea na kesi hiyo.
 
Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana, zilisema kuwa viongozi kadhaa wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa, wajumbe wa Kamati Kuu na wabunge kadhaa wa chama hicho tayari walikuwa wamewasili mjini Dodoma.

Hata hivyo, akizungumzia kesi hiyo, Lissu alisema kuwa hatakubali ‘withdrawal’ isipokuwa anataka ‘dismiss with cost’.

Lissu alisema kuwa Wasonga atalazimishwa kulipa gharama kwa kuwa hati ya kiapo cha Selema ni ya mwezi Juni 25, mwaka huu, na kwamba kutaka kuiondoa siku mbili kabla ni uhuni.
 
Shabani Selema na Paskali Hallu ni wanachama wa CCM wakazi wa kijiji cha Makiungu, mkoani Singida, ambao walifungua kesi ya msingi ya kupinga ubunge wa Lissu.
 
Lakini baada ya hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kumtangaza Lissu kama mbunge halali, walikubaliana na hukumu hiyo ya Aprili 27, mwaka huu.
 
Mara kadhaa wananchi hao wamenukuriwa wakimlalamikia Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kuwa anawashinikiza kuendelea na rufaa hiyo licha ya kwamba walishajitoa.
 
Akizungumza na gazeti hili juzi, Wasonga, ambaye alikuwa akiwatetea wanachama hao katika kesi hiyo, alisema kuwa baada ya kuwasiliana na wateja wake walimwambia hawakuwa tayari kuendelea na kesi hivyo.
 
“Ni kweli walalamikaji wote wamejitoa na mimi kama wakili sioni haja ya kuendelea; nitakuwa namwakilisha nani?
“Niliongea nao jana hakuna; mwenye nia ya kuendelea na kesi,” alisema.
 
Rufaa hiyo imepangiwa kusikilizwa katika Mahakama ya Rufani na Jopo la Majaji watatu, Salumu Massati, Engela Kileo na Natalia Kimaro.
 
Kabla ya kuanza kusikilizwa kwa rufaa hiyo, mahakama ilitarajiwa kusikiliza pingamizi zilizotolewa na upande wa walamikiwa ambao ni Lissu na jamuhuri za kupinga rufaa hiyo na jopo hilo la majaji litatoa maamuzi.
 
Tayari Lissu alitoa hoja saba za kupinga rufaa hiyo, ambazo ni mkata rufaa Seleman ambaye ndiye mlalamikaji namba moja kupinga kwamba hajakata rufaa kwa hati ya kiapo ya Mei 24 mwaka huu.
 
Alisema hoja nyingine ni notisi ya kiapo kutopelekwa kwa mjibu rufaa ambaye ni yeye kinyume na masharti ya kanuni ya 84 (1) ya Kanuni za Adhabu za Mahakama ya Rufaa Tanzania za mwaka 2009.
 
“Vile vile nakala zote rekodi za rufaa hazijathibitishwa usahihi wake na wakata au wakili kinyume na masharti ya Kanuni ya 96 (5) ya Kanuni za Mahakama ya Rufaa Tanzania za mwaka 2009.
 
“Rufaa hii pia imepitwa na muda wake kwa sababu hati ya ucheleweshaji iliyotolewa na Msajili wa Mahakama Kuu haijasainiwa, haina tarehe wala muhuri kinyume na Kanuni ya 90 (1) ya Kanuni za Mahakama ya Rufaa ya Tanzania za mwaka 2009,” alisema.
 
Lissu aliongeza kuwa walalamikaji walitakiwa kukata rufaa siku sitini baada ya notisi ya rufaa kutolewa na kwamba tarehe ya mwisho ya kukata rufaa ilikuwa Julai 3 mwaka jana lakini rufaa hiyo ilikatwa Mei 7 mwaka huu.
 
“Hoja nyingine ni kwamba rufaa hiyo si halali kwa kuwa imeacha nyaraka muhimu ikiwemo maombi ya mwenendo wa shauri wa kusamehewa gharama za dhamana,” alisema.

Lissu alisema pia katika rufaa hiyo, amri iliyomshindisha kesi si halali kwa kuwa haionyeshi tarehe ambayo amri hiyo ilitolewa kinyume na kanuni ya 9 ya Kanuni za Masijala za Mahakama Kuu za mwaka 2005.
 
Alisema pia wakata rufaa wamesindwa kuwasilisha mahakamani hoja za maandishi za kuunga mkono hoja za rufaa yao ndani ya siku 60 au kuomba muda wa kuziwasilisha.
 
Pia hoja nyingine ni kushindwa kuwasilisha hoja hizo za maandishi kinyume cha Kanuni ya 106 (1), (2) na (9) ya Kanuni za Mahakama ya Rufaa ya Tanzania za mwaka 2009.
 
Kesi ya kupinga ubunge wa Lissu ilianza kusikilizwa Machi 12, 2012 na Jaji wa Mahakama Kuu, Moses Mzuna, aliyetoa hukumu April 27, mwaka huu, na kumtangaza Lissu kuwa mbunge halali wa Singida Mashariki kwa kigezo kuwa hoja zote zilizotolewa na wanachama hao wa CCM hazitoshi kutengua au kubatilisha ubunge wake.

-Tanzania Daima

Wednesday, 11 September 2013

POLISI MKOANI DODOMA YASHINDWA KUMFIKISHA MAHAKAMANI MBUNGE SUGU WA MBEYA MJINI


JESHI la Polisi mkoani Dodoma limeshindwa kumpandisha kizimbani Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kwa madai kuwa upelelezi bado haujakamilika. Mbilinyi, maarufu kama ‘Sugu’ alifunguliwa jalada na jeshi hilo Ijumaa iliyopita, akidaiwa kumjeruhi jichoni askari wa Bunge, Koplo Nikwisa Nkisu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Wakili wake, Tundu Lissu, alisema kuwa hawakufikishwa mahakamani kama walivyotegemea kutokana na kuelezwa kuwa upelelzi haujakamilika.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema kuwa baada ya mteja wake kuripoti kituoni aliambiwa kwamba upelelezi huo ukikamilika wataitwa ili kupewa maelezo ya hatua gani inafuata.
Alisema kitendo hicho cha polisi kuwaita bila kukamilisha upelelezi wao ni kuwapotezea muda.
“Nashangaa ni kwanini tunaitwa, tuliambiwa tufike hapa, lakini tulipokuja hapa hakuna jambo lolote la maana tuliloambiwa, badala yake wanasema tuendelee na shughuli zetu upelelezi haujakamilika na baada ya wiki mbili watatuambia kinachoendelea.
“Yaani, haya mambo yanayofanywa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi na Naibu wa Spika, Job Ndugai, ni ya ajabu sana. Tumeitwa kutoka mbali kote kwa ajili ya kuja hapa kuambiwa kuwa upelelzi haujakamilika,” alisema.
Aliongeza kuwa Sugu alitoka Mbeya huku naye akitoka huko alikokuwa kwa ajili ya kuja Dodoma lakini hakuna jambo lolote limefanyika, na kuhoji ni kwanini wasingearifiwa hata kwa simu.
Lissu alisema kuwa atashanga kama jeshi hilo litapeleka kesi hiyo mahakamani kwani kosa lenyewe lilifanyikia bungeni.“Nitashangaa kama jambo hili litapelekwa mahakamani, kwani kwa mujibu wa kanuni, mbunge hatashitakiwa kwa jambo ambalo alilitenda akiwa katika maeneo ya Bunge.
“Mambo haya yalitokea tukiwa bungeni na huko kuna kinga ya mbunge. Mbunge akikosa anahukumiwa kwa mujibu wa kanuni, lakini kwa fikra na mashikinizo ya viongozi wa CCM wanataka kuvuruga na kufanya mambo kwa masilahi ya chama chao,” alisema.
Naye Sugu alisema kuwa kitendo kilichofanywa na Ndugai ni cha kihuni na wala hakikuwa na misingi yoyote hadi kulazimisha askari wa Bunge kumpiga.

NDUGAI NA MBOWE WALIVUNJA SHERIA ZA BUNGE MAKUSUDI KWA MASLAHI YA VYAMA VYAO


Kumekuwa na mjadala mkali kuhusu iwapo Naibu Spika, Job Ndugai alikiuka Kanuni za Bunge katika kushughulikia vurugu zilizotokea Bungeni Alhamisi iliyopita kwa kuamuru kutolewa nje kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe. 


Ndugai ambaye alikuwa kiongozi wa shughuli za Bunge siku hiyo, aliwaamuru askari kumtoa nje Mbowe baada ya kukaidi amri yake ya kutaka kuketi chini aliposimama kutaka kupewa nafasi ya kuzungumza, hali iliyozua tafrani bungeni.
 

Pamoja na mambo mengine Ndugai amekuwa akituhumiwa kwamba anaminya uhuru wa wabunge wa upinzani kutokana na mapenzi aliyonayo kwa chama chake, CCM.
 

Kwa upande mwingine, kumekuwa na lawama kwamba Mbowe alikosea kukaidi amri ya Naibu Spika kwa kuwa kanuni zinamtaka mbunge yeyote (hata akiwa waziri), kuketi pale kiongozi wa Bunge (Spika, Naibu au Mwenyekiti) anaposimama, hivyo kusababisha mtafaruku.
 

Mwenyekiti wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, Profesa Chris Peter Maina alisema tatizo lililojitokeza bungeni linaweza kumalizwa na kuwapo kwa sheria inayokataza Spika wa Bunge kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa.
 

“Unajua kwa Katiba ya sasa Spika wa Bunge anaweza kuwa mwadilifu lakini akapata shinikizo kutoka upande wa chama chake, Ibara ya 128 ya Rasimu ya Katiba Mpya inaeleza kiundani kuhusu spika kutokutoka miongoni mwa wabunge jambo ambalo ni zuri,” alisema Profesa Maina na kuongeza:
 

“Mwenendo wa Bunge siyo mzuri. Wabunge hawaheshimiani hata kidogo, nadhani wanahitaji kukubaliana kwa hoja, wao ndiyo wanatunga sheria, hivyo wanatakiwa kulumbana kwa kufuata utaratibu uliowekwa.”
 

Spika wa zamani, Pius Msekwa alisema wakati akiongoza Bunge hakuwahi kuona vurugu, fujo na malumbano ya wabunge kama ilivyotokea Alhamisi iliyopita.
 

“Wakati nikiwa Spika sikumbuki kama kuna siku ziliwahi kutokea vurugu za aina hii, kilichotokea ni sawa na uhalifu kwa sababu taratibu hazikufuatwa,” alisema Msekwa.


Matakwa ya Kanuni

Ibara ya 76 (1) na (2) ya Kanuni za Bunge Toleo la Aprili 2013, zinaeleza jinsi ya kudhibiti fujo bungeni, lakini Ndugai anakosolewa kwamba hakuzingatia taratibu hizo kushughulikia vurugu za Alhamisi.
 

Kanuni ya 76 (1) inasema: “Kwa madhumuni ya kudhibiti fujo endapo itatokea ndani ya Ukumbi wa Bunge na Spika ataona kuwa kuna haja ya kutumia nguvu, basi anaweza kuahirisha shughuli za Bunge bila ya hoja yoyote kutolewa au kusitisha kikao kwa muda atakaoutaja ili fujo hiyo iweze kudhibitiwa na Mpambe wa Bunge”.

Kadhalika, fasili ya pili ya Kanuni hiyo inasema: “Baada ya utulivu kurudia, Spika atalipeleka kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge suala ambalo lilisababisha kutokea kwa fujo ikiwa ni pamoja na jina la mbunge au majina ya wabunge waliohusika na fujo hiyo ili kamati hiyo iweze kulishauri Bunge kuhusu adhabu inayostahili kutolewa”.
 
Wakati vurugu zilipozuka bungeni, Ndugai aliwaita askari badala ya mpambe, kumtoa nje Mbowe na hakuwa amesitisha wala kuahirisha shughuli za Bunge kama kanuni zinavyotaka.
 
Pia Naibu Spika alitangaza kumsamehe Mbowe na Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kwa maana ya kuwaruhusu kuendelea na vikao vya Bunge siku hiyo jioni, badala ya suala hilo kupelekwa kwenye kamati husika kama kanuni ya 76 (2) inavyoelekeza.
 
Utetezi wa Ndugai
Ndugai alisema hakuzingatia kanuni hizo kwani mazingira ya vurugu hizo hayaendani na kanuni husika, hivyo alitumia nafasi yake ambayo pia inatambuliwa na kanuni za Bunge.
 
“Vurugu zilikuwa zimepangwa na zilifanywa kwa makusudi ili kuhakikisha kwamba shughuli za Bunge zinakwama maana hiyo kanuni wanafahamu kwamba ipo, sasa hatuwezi kuwa na Bunge ambalo mtu akiamua tu anafanya fujo ili liahirishwe,” alisema Ndugai na kuongeza:
 
“Mimi kama kiongozi wa shughuli za siku hiyo, kazi yangu ni kuhakikisha kwamba shughuli zilizopangwa zinafanyika, kwa hiyo nisingeweza kuruhusu watu wachache watukwamishe kutokana na masilahi yao.”
 
Alipoulizwa kwamba alifahamu vipi kuwapo kwa njama hizo, alisema kauli na matendo ya wabunge wa upinzani vilionekana tangu mwanzo wa mjadala kutaka kukwamisha shughuli za Bunge siku hiyo.
 
Kuhusu kuwatangazia wabunge hao msamaha badala ya kupeleka suala hilo kwenye kamati husika, Ndugai alisema: “Hakukuwa na adhabu kubwa ya kuwapa zaidi ya kuwatangazia msamaha.”
 
“Niliwasamehe kwa mujibu wa kanuni maana zinaruhusu kuzingatia uamuzi ambao uliwahi kutolewa na maspika waliopita, kwa hiyo kama unakumbuka kesi ya Mengi (Regnald) na Malima (Adam), Spika Samuel Sitta baada ya kumwita Malima akakataa kwenda alisema anamsamehe,” alisema na kuongeza:

“Yeye (Sitta) alitumia neno kwamba nimeamua kumpuuza lakini mimi sikusema hivyo, nilisema kwamba namsamehe kwa sababu tu namheshimu na ni kiongozi mkubwa tu katika jamii”.
 
Lissu amtetea Mbowe
Mbowe hakupatikana juzi na jana kuzungumzia suala hilo, lakini Mnadhimu Mkuu wa Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alisema kiongozi wake huyo hakufanya makosa kwani alisimama wakati Mbunge wa Vunjo (TLP), Augustine Mrema alipokuwa akizungumza na kwamba hilo siyo kosa kikanuni.
 
Alisema Ndugai alipaswa kumheshimu Mbowe kwa kuzingatia wadhifa wake bungeni na kwamba kitendo cha kumwambia “kaa chini” hakikubaliki.
 
“Hatuwezi kuruhusu na hatutaruhusu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kudhalilishwa, ikiwa tutaruhusu hilo litokee, basi miongoni mwetu sisi wapinzani hakuna atakayepona,” alisema Lissu na kuongeza:
 
“Naibu Spika amelidhalilisha Bunge kwa sababu kwa kumdharau Mbowe ni kwamba amemdharau mmoja wa viongozi wakuu wa Bunge”.

-Mwananchi

Tuesday, 10 September 2013

JALADA LA KESI YA MBUNGE SUGU LATUA KWA DPP MBEYA


JALADA la Kesi inayomkabili Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), limefikishwa katika Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali. Mbilinyi maarufu kwa jina la ‘Sugu’, anadaiwa kumjeruhi askari wa Bunge katika vurugu zilizotokea Bungeni mwishoni mwa wiki iliyopita. 

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Susan Kaganda alisema polisi wameshapeleka jalada la mbunge huyo katika Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali na kwamba upelelezi unaendelea.

“Tayari jalada la kesi yake lipo katika Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali na upelelezi unaendelea,” alisema.

Kwa mujibu wa vyanzo kutoka Jeshi hilo, Sugu alikwenda Polisi kujisalimisha siku ya kuahirishwa Bunge na kwamba aliambiwa arudi tena kuripoti Jumatano (kesho). “Kama akiripoti Jumatano, ndiyo itajulikana na kama jalada lake litakuwa limeshafikishwa mahakamani au bado,” kilieleza chanzo hicho.

Habari za uhakika kutoka katika Mahakama ya Mkoa wa Dodoma hadi jana mchana, hakukuwa na jalada lolote lililokuwa limefika mahakamani linalomuhusu Sugu. “Kwa leo (jana), majalada yaliyopokelewa hadi sasa ni mawili tu na yote yanahusu ‘Trafiki kesi’ kilieleza chanzo hicho.

Kusakwa kwa mbunge huyo kulitokana na vurugu zilizotokea katika ukumbi wa Bunge ambao uligeuka ulingo wa masumbwi, baada ya wabunge wa kambi ya upinzani kupigana hadharani na askari wa Bunge.

Wabunge hao walichapana ndani na nje ya ukumbi, hali iliyosababisha tafrani kubwa, huku maofisa usalama na askari polisi kutoka kituo kikuu mjini Dodoma, wakilazimika kuitwa kwenda kuongeza nguvu ili kukabiliana na hali hiyo.

Hatua ya vurugu hizo, ilikuja baada ya Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kunyanyuka ili kutaka kutoa hoja, ambapo Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alimtaka kukaa chini hali iliyowafanya wabunge wote wa upinzani kunyanyuka wakiashiria kumuunga mkono.

Katika vurugu hizo, ‘Sugu’, inadaiwa alimpiga kichwa, ngumi na kumjeruhi jicho la upande wa kulia Koplo Nikwisa Nkisu.

Chanzo cha vurugu hizo ni madai ya wabunge kutoka vyama vya Chadema, CUF na NCCR- Mageuzi kutaka kuahirishwa kwa Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kwa kuwa mchakato wa kuandaliwa kwake haukuwashirikisha Wazanzibari. 


-Mtanzania

SIO SIRI TENA,MMILIKI WA WA MELI ILIYOKAMATWA ITALIA IKIWA NA MAGUNIA TANI 30 YA BANGI NI MBUNGE WA TANZANIA

Magunia ya bangi japo siyo yaliyokuwa katika MV Gold Star.
 USIRI ulikuwa umetawala kuhusu mmiliki wa meli ya Kitanzania iliyonaswa juzi nchini Italia, ikiwa na tani 30 za madawa ya kulevya aina ya bangi lakini sasa kila kitu kinaweza kuwekwa nje bin hadharani kutokana na taarifa mpya.
 
Mv Gold Star ikiungua.
tunazo ‘data’ kuwa mmoja wa wamiliki wa meli hiyo ni mfanyabiashara wa Kitanzania mwenye asili ya Bara la Asia ambaye alipata kuwa memba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu zilizopita.
Jina la mfanyabiashara huyo linabaki kwenye kapu letu mpaka baadaye tutakapokuwa kwenye mazingira sahihi ya kumtaja, kwani kufanya hivyo kwa sasa ni kuingilia mamlaka za kisheria ambazo zipo kwenye uchunguzi makini.
Habari zinafafanua kuwa mbunge huyo, hamiliki meli hiyo peke yake, bali kuna watu wengine ambao ni raia wa Visiwa vya Marshall, barani Australia.
Magunia ya bangi japo siyo yaliyokuwa katika MV Gold Star.
Inaelezwa zaidi kwamba watu hao kutoka Marshall ni mabilionea wakubwa ambao wanamiliki visiwa vitatu kwenye Bahari ya Pacific ambavyo ni Ujae Atoll, Ujelang Atoll na Lib.
Mabilionea hao ndiyo wenye Kampuni ya Gold Star Shipping ambayo inajihusisha na utoaji wa huduma za usafiri wa majini hususan kwa njia ya meli.
Gold Star Shipping ni kampuni iliyosajiliwa Visiwa vya Marshall lakini kwa ushirikiano na mbunge huyo wa zamani, waliileta nchini meli yao ya mizigo ya MV Gold Star, ikasajiliwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

MAGUMASHI YALIPOANZA
MV Gold Star ilisajiliwa Zanzibar ili tu ipate kibali cha kutumia Bendera ya Taifa la Tanzania, kwani baada ya hapo, imekuwa ikipuyanga kwenye mataifa mengine, ikitoa huduma za usafiri pasipo kurudi kwenye nchi iliyosajiliwa.
Taarifa za hivi karibuni, zinaonesha kuwa imeshakwenda na kurudi Misri mara mbili, Algeria mara mbili na Uturuki, huku Bandari ya Zanzibar ambayo inaitambulisha kama ndiyo nyumbani kwao, haijapata kutia nanga hata mara moja.
Julai 29, 2013, saa 2:04 asubuhi, ilitia nanga Bandari ya Said, Misri. Juni 18, 2013, saa 1:05 jioni, iliwasili Bandari ya Mostaganem, Algeria. Mei 31, 2013, saa 9:04 usiku, ilifika Bandari ya Iskenderun, Uturuki. Mei 24, 2013, saa 1:04 asubuhi, iliingia Bandari ya Said, Misri na Aprili 14, 2013, saa 2:02 asubuhi, ilipiga king’ora Bandari ya Mostaganem, Algeria.

WASIFU WA MELI
Bandari ya nyumbani ni Zanzibar, imetengenezwa mwaka 1975, watengenezaji ni Kampuni ya Astilleros De Mallorca, iliyopo Palma De Mallorca, Hispania, mmiliki ni Gold Star Shipping kutoka Visiwa vya Marshall, meneja ni Gold Star Shipping, ipo katika jamii ya Hellenic Shipping Register.

WAMILIKI WA ZAMANI
Ilimilikiwa na Ibrahim Junior mpaka Februari 2011, Breogan I (aliiuza Novemba 2006), Breogan (Machi 2002), Estela De Mar (Desemba 1996), Inezgane (1996), Puerto Suances (1988) na Suecia (1985).

NI MADAWA YENYE THAMANI KUBWA
Kwa mujibu wa ripoti za mitandao ya Waitaliano na Waingereza, MV Gold Star, ilipakia mzigo wa madawa ya kulevya nchini Uturuki na walikuwa wanafanya jaribio la kuingiza mzigo huo wenye tani 30 nchini Italia.
Walinzi wa ufukweni kwenye Bahari ya Mediterranean, waliishtukia meli hiyo na kuizingira, watu waliokuwemo baada ya kuona hali ni mbaya, waliwasha moto kuiteketeza MV Gold Star kisha kufanya jaribio la kutaka kutoroka kupitia boti ndogo.
Askari hao wa ufukweni, walishirikiana na maofisa uhamiaji wa Italia kuwakamata watu tisa ambao walikuwemo kwenye meli hiyo na baada ya kuwahoji, ilibainika wote wanatokea nchi za Misri na Syria.
Taarifa kutoka kwa maofisa uhamiaji wa Italia zinasema kwamba baada ya kuwahoji watuhumiwa, ilibainika waliamua kuiteketeza meli hiyo kwa moto ili kuondoa ushahidi wa tani 30 za madawa ya kulevya zilizokuwemo.
Ilibainishwa pia kuwa thamani ya madawa hayo ya kulevya yaliyokamatwa ni pauni milioni 50 ambazo kwa chenji ya Tanzania ni shilingi bilioni 126.5.

FEDHA HIZO ZINAWEZA KUENDESHA WIZARA TATU
Kama mzigo huo ungevuka salama na kuuzwa, fedha hizo zinatosha kuendesha wizara tatu katika Serikali ya JK, hii ni kwa mujibu wa makadirio na mapato ya matumizi (bajeti), mwaka wa fedha 2013-2014.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto bajeti yake ni shilingi bilioni 23, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo shilingi bilioni 30 na Wizara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mifugo shilingi bilioni 67, jumla shilingi bilioni 120.
Hii inamaanisha kuwa fedha hizo za wauza unga, zinaweza kuendesha wizara hizo na chenji itabaki shilingi bilioni 6.5 ambazo zinaweza kujenga shule na mabweni mengi tu. Uchambuzi huo ni kuonesha namna ambavyo wauza unga walivyo watu hatari, kwani wana pesa nyingi.

ITALIA KAZI WANAYO
Baada ya kuwakamata watuhumiwa hao, vikosi vya uokoaji nchini humo, kuanzia vya majini, anga na nchi kavu, viliizingira meli hiyo kuzima moto uliokuwa unaiteketeza.
Mpaka tunakwenda mitamboni, taarifa zilieleza kwamba bado shughuli ya kuzima moto ilikuwa inaendelea.

TANZANIA HAKUNA ANAYEJUA
Tuilifanya jitihada za kuwatafuta watu mbalimbali wanaohusika na udhibiti wa madawa ya kulevya nchini lakini hakuna hata mmoja aliyekuwa na taarifa.
Hata Kamanda wa Kikosi cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya, Godfrey Nzowa, aliliambia  akiwa nchini Ethiopia kuwa hajui chochote kuhusu meli hiyo kukamatwa lakini aliahidi kufuatilia.

NI SKENDO NZITO KWA NCHI
Kukamatwa kwa meli hiyo kunazidi kuipaka matope Tanzania, kwani hivi karibuni raia wake wamekuwa wakikamatwa katika mataifa mengine, wakiwa wanasafirisha madawa ya kulevya. Vilevile, kuna ile skendo ya meli ya Wairan yenye Bendera ya Tanzania ambayo iliibua gumzo mwaka huu lakini suluhisho halijapatikana. 
-GPL

Monday, 9 September 2013

NDUNGAI ATAJA SABABU ZAKE ZILIZOFANYWA AMTIMUE FREEMAN MBOWE BUNGENI


NAIBU Spika, Job Ndugai ametetea uamuzi wake wa kuagiza kutolewa ndani ya ukumbi wa Bunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akisema alikuwa sahihi.

Mabishano hayo ambayo yalisababisha kuibuka kwa vurugu bungeni yalitokea mwishoni mwa wiki, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu, ambapo kiongozi huyo wa Bunge aliruhusu mjadala kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba uendelee.

Kutokana na hali hiyo, Mbowe alisimama kutaka kutoa ufafanuzi juu ya mjadala huo, lakini Ndugai alimzima na kumtaka kukaa chini, jambo ambalo halikumfurahisha Mbowe na kumfanya agomee agizo lake.

Akizungumza na MTANZANIA jana kwa njia ya simu, Ndugai alitumia muda mwingi kutetea uamuzi wake na kukosoa hoja za watu wanaompinga juu ya uamuzi wake huo.

Ndugai alisema katika kikao hicho, Mbowe alifanya jeuri kubishana na kiti na kueleza kuwa kanuni za Bunge zinasema hakuna mbunge yeyote atakayesimama kuzungumza bila kuruhusiwa na kwamba uamuzi wa kiti ndiyo wa mwisho.

Ndugai alisema wanaomtuhumu kwamba hakutenda haki kumuamuru Mbowe akae chini, wanafanya hivyo kwa vile hawajui kanuni za Bunge.

Ndugai alisema kwa mujibu wa kanuni, ni Rais wa Jamhuri pekee ndiye anayeruhusiwa kulihutubia Bunge kwa wakati anaoona yeye unafaa, lakini si mbunge.

“Hata rais mwenyewe ni lazima amwandikie barua spika, huu ndiyo utaratibu lakini si mbunge au waziri anayeruhusiwa kusimama kwa wakati anaoutaka yeye kuzungumza akaruhusiwa, ni lazima ataomba ruhusa kwa Spika na kama ipo nafasi ya kufanya hivyo Spika atamruhusu, kama haipo hataruhusiwa.

Alipoulizwa kwamba haoni kama alivunja kanuni kwa kumzuia Kiongozi wa Upinzani bungeni wakati kanuni za mabunge ya Jumuiya ya Madola zinatoa upendeleo kwa kiongozi huyo na waziri mkuu ndani ya Bunge, Ndugai alisema:

“Katika vikao vya Bunge, uamuzi wowote wa Spika unakuwa wa mwisho na hauwezi kupingwa na mbunge au waziri yeyote.

“Mbowe nilimuomba kwa heshima sana atupishe kwanza, nilimuelekeza karibu mara tatu…lakini mtu mzima anavunja utaratibu.

“Huyu Mbowe amejivunjia heshima mwenyewe, hata kanisani anayeendesha ibada ni mtu mmoja tu, na wengine wanapaswa kufuata utaratibu.

“Kwanza Mbowe alijitoa mwenyewe kwenye orodha kwa maandishi na ninayo hapa.... yeye na Halima Mdee, sasa alisimama kufanya nini kama sio ujeuri?

“Kanuni anazijua mimi ningemruhusu tu, lakini kwa ujeuri hakufanya hivyo. Kuna taratibu za bunge, mbunge anakaa chini pale Spika anaposimama na wasome kanuni, sasa hapo mjeuri ni nani?

“Tujifunze kanuni haiwezekani mtu yeyote asimame saa yoyote, kila mmoja hawezi kufanya anavyotaka, kuna taratibu zake, kiti kikimuona atapewa nafasi kama ipo na iwapo kiti kikiridhika,” alisema Naibu Spika.

Awatetea askari wa Bunge

Akizungumzia hatua ya kuwaamuru askari wa bunge kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge na kumtoa Kiongozi wa Upinzani, iwapo kama amevunja kanuni, Ndugai alisema hakuvunja kanuni na kufafanua kila askari aliye kwenye viunga vya bunge yuko chini ya himaya ya kiti.

“Kila askari aliye kwenye eneo la bunge au viunga vya bunge kuanzia polisi, usalama wa taifa na wengine wote siwezi kuwataja hapa, hao wote wako chini ya bunge ni Sajent at Arms.

“Askari polisi wote unaowaona bungeni wanaletwa na RPC Dodoma na wanakuwa chini yetu, hakuna askari aliyetoka nje siku ile…. Ni uongo na hawajui kanuni.

“Uamuzi wa kuita wanausalama ndani ya ukumbi ulikuwa ni uamuzi sahihi, hakuna askari aliyetoka nje ya bunge,” alisisitiza Ndugai.

Msekwa amuunga mkono Ndugai

Naye Spika Mstaafu aliyeongoza Bunge la nane, Pius Msekwa alimtetea Ndugai akisema kuwa haoni kosa lolote lililofanywa na kiongozi huyo wa Bunge.

Msekwa ambaye alipata kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), alisema ni jambo la kawaida ndani ya Bunge, Spika kumuamuru mbunge au waziri kukaa chini pale anapoona inafaa.

“Spika ni sawa na mwenyekiti wa kikao chochote, anayo madaraka ya kuruhusu nani aseme, nani asiseme.

“Tuje bungeni sasa, Ndugai ndiye anayeamua nani aseme, ni sahihi ndiye mwenye mamlaka hayo na ni jambo la kawaida kabisa,” alisema Msekwa.

Akitoa uzoefu wake wa bunge alilokuwa akilisimamia, Msekwa alisema matukio yanayotokea bungeni sasa yamegubikwa na hisia za ujana zaidi na kusisitiza wazee walio nje ya bunge wanatafakari cha kufanya kabla hali haijaharibika.

“Sisi yetu macho… lakini kila zama na kitabu chake, hizi ndio zama za vijana, wakati wetu haya hayakuwapo…lakini ikifikia hatua ya kutaka kuliteketeza bunge lazima tutachukua hatua… lakini dalili sio nzuri,” alisema Msekwa.


-Mtanzania

Friday, 6 September 2013

HIZI NDIO PICHA ZA TUKIO ZIMA YA KULICHOJIRI JANA BUNGENI

1920241816121514131717232222211214

WANANCHI WALILAANI BUNGE LA TZ KUTOKANA NA VURUGU ZINAZOENDELEA



Baada ya kuibuka mvutano mkali bungeni jana, kati ya Naibu Spika, Job Ndugai na wabunge wa Kambi ya Upinzani, wasomi, wanaharakati, Chama cha Madaktari Tanzania (Mat), Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), vimesema kinachoendelea sasa ndani ya Bunge ni masilahi ya vyama vya siasa siyo taifa.


Walitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya Naibu Spika, Job Ndugai kuwataka askari kumtoa nje ya Ukumbi wa Bunge, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.


Mbowe aligoma kukaa chini na kuungwa mkono na wabunge wa upinzani, akishinikiza kuahirishwa kujadiliwa kwa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, hadi hapo Zanzibar itakaposhirikishwa, muda mfupi baada ya wabunge kupiga kura na 156 kutaka ujadiliwe na 56 wakitaka uondolewe.


Wabunge hao wa upinzani kutoka vyama vya Chadema, CUF na NCCR- Mageuzi, juzi walitoka nje ya Ukumbi wa Bunge wakishinikiza kuahirishwa kujadiliwa kwa muswada huo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema mvutano huo umejaa masilahi ya wanasiasa kwa kila upande kujaribu kuvutia kwake.


“Mvutano ule hauzungumzi kabisa mwafaka wa Bunge la Katiba, binafsi nadhani Bunge la Katiba linatakiwa kuwa na wabunge wapya kabisa na wasiotoka katika chama chochote cha siasa,” alisema


Katibu Mkuu wa Tucta, Nicolaus Mgaya alisema: “Marekebisho hayo yanafanyika kwa ajili ya mustakabali wa Muungano wetu, kama Zanzibar hawakushirikishwa, uwekwe utaratibu wa jambo hilo kufanyika ili kipatikane kitu bora, siyo bora Katiba.”


Alisema nchi zilizoendelea zimepata mafanikio kwa kuwa zina Katiba nzuri ambazo zinaweza kudumu kwa miaka 100 kabla ya kufanyiwa marekebisho..

Thursday, 5 September 2013

RIPOTI MAALUMU YA GAZETI LA MWANANCHI KUHUSIANA NA VURUGU ZILIZOTOKEA JANA BUNGENI

 
           Jana, Bingwa wa Dunia wa uzani wa kati (super middle), unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF), Francis Cheka alitembelea Bunge baada ya kutwaa taji hilo karibuni na jana hiyohiyo, Bunge hilo lilishuhudia ngumi kavukavu katika vurugu kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kutokea katika ukumbi wake.


Katika masumbwi hayo yasiyo rasmi, Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ anadaiwa kumpiga kichwa Askari wa Bunge na kumchania sare na kung’oa kipaza sauti.



Mbilinyi jana alisema alikuwa anatafutwa na polisi huku akisema hilo limemshangaza akidai kwamba yeye ndiye aliyeshambuliwa na askari huyo.


Vurugu hizo zilitokea baada ya Naibu Spika, Job Ndugai kuamuru kutolewa nje kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.


Katika vurugu hizo Mbilinyi alibebwa juujuu na polisi hadi nje ya ukumbi huku akiwa hana viatu.


Pamoja na tafrani hiyo, Ndugai alisema wakati akihitimisha kikao cha Bunge kipindi cha asubuhi kuwa amewasamehe wabunge wote waliohusika na kosa hilo la utovu wa nidhamu na kuwaruhusu kurejea kipindi cha jioni kuendelea na Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. 

Hata hivyo, wabunge wote CUF, NCCR-Mageuzi na Chadema ambao baada ya tukio hilo walitoka nje ya ukumbi, hawakurejea na baadaye walitoa msimamo wa pamoja wakisema hawatashiriki katika mjadala huo.


Msimamo huo ulitolewa na Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Mbunge wa CUF, Habib Mnyaa.


Mbowe alisema wameamua kususia majadiliano hayo kuonyesha msimamo wao wa kupinga kupitisha mambo yasiyo na masilahi kwa nchi.
 
“Hatuko tayari kushiriki katika uchakachuaji wa Katiba... Matumizi ya nguvu ya polisi kamwe hayatatupatia Katiba nzuri,” alisema. Alisema kambi rasmi ya upinzani inalaani vikali kitendo cha Ndugai kuruhusu Bunge kunajisiwa kwa kuruhusu polisi kuingia ndani kinyume na kanuni.


Mnyaa alisema kitendo cha wadau wa Zanzibar kutoshirikishwa katika kutoa maoni yao katika muswada huo wa marekebisho ni dharau kubwa.


Mbatia alisema Tanzania haiwezi kuingia Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa kutumia Katiba ya sasa kwa sababu tayari kuna mgongano wa kikatiba kati ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alimtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kutoa ushahidi kama Rais aliteua wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kulingana na mapendekezo ya taasisi zao.

Kuanza kwa tafrani
Sakata hilo lilianza saa 6:45 mchana muda mfupi baada ya kukamilika kwa kura kuamua kama Bunge liahirishwe au la kutokana na hoja iliyotolewa na Mbunge wa Mkoani (CUF), Ali Hamisi Seif (CUF). Waliotaka liahirishwe walipata kura 59 na waliokataa 159.

Baada ya Ndugai kutangaza matokeo hayo na kutaka shughuli za Bunge ziendelee, Mbowe aliposimama na kusema ana hoja Naibu Spika alimwamuru akae chini.

Baada ya Mbowe kusisitiza ana hoja na kumwomba Spika amsikilize ndipo Ndugai alipomwamuru atoke nje na alipokaidi alisema:” Naomba askari wote waliopo katika mazingira haya (ya Bunge) waingie ndani ya ukumbi wa Bunge”.

Baada ya kitambo kifupi, Mbowe akiwa bado amesimama alitoa maagizo atolewe nje: “Kiongozi wa upinzani atolewe nje.”

Polisi waliingia ndani ya Ukumbi wa Bunge lakini Wabunge wa Kambi ya Upinzani kwa umoja wao, walimzinga Mbowe asifikiwe na askari hao.

Baada ya kuona polisi wanaelekea kushindwa, Ndugai alitoa maagizo mengine: “Askari hamjaletwa humu ndani kufanya majadiliano mnatakiwa kuhakikisha kiongozi wa upinzani anatolewa nje”.

Alisema yeye ndiye anayeendesha kikao hicho hivyo lazima Mbowe atolewe nje.

Hapo ndipo wabunge hao wa upinzani walipoanza kuimba: “Hatutaki kuburuzwa hatutaki kuburuzwa… hatutaki kuonewa,” huku wakiendelea kumzinga Mbowe.

“Askari wote mliopo humu ndani naomba mnisikilize… Sasa naagiza kwa mara ya mwisho... nasema kiongozi wa upinzani atolewe nje.”

Ngumi zarushwa
Baada ya kauli hiyo ya Ndugai, ndipo polisi walipotumia nguvu hasa kwa Mbilinyi na Mbunge wa Maswa Mashariki (Chadema), Silvester Kasulumbai.

Katika patashika hiyo, inadaiwa kwamba Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali alipigwa ngumi ambayo ilimfanya apepesuke hadi sakafuni.

Kilichomponza Mbilinyi ni hatua yake ya kusogelea Siwa. Polisi waliokuwa karibu, walimbeba juujuu hadi nje ya ukumbi.

Wakati akitolewa nje ya ukumbi, alijaribu kujizuia kwa kushika kipaza sauti kinachotumiwa na upande wa upinzani hadi kikang’oka.

Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Mozza Abeid, alivuliwa hijabu katika vurumai hizo wakati polisi walipokuwa wakitumia nguvu ili kumfikia Mbowe.

Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, Mbowe aliamua kutoka nje huku akisindikizwa na polisi pamoja na wabunge wa vyama hivyo na alipofika nje ya ukumbi alipokewa na polisi wa kawaida waliomweka chini ya ulinzi kabla ya kumwachia baada ya ombi la Mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini.

Kutokana na hali ya mambo kuwa tete, askari wa Bunge waliwaondoa wageni waliokuwa wamekaa katika kumbi za wageni wakiwamo wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari huku baadhi ya wabunge wa CCM waliokuwa na simu za kisasa za mkononi na kompyuta mpakato (Ipad) wakichukua picha za tukio zima.

Inadaiwa kwamba baada ya kutoka nje ya ukumbi, Mbilinyi alimtwanga ngumi mmoja wa askari waliomtoa kwa nguvu kabla ya kuamuliwa na wabunge na polisi.
Wakati wote huo, wafanyakazi wa Bunge na wageni walionekana wakiwa wamejikusanya katika makundi wakitafakari na kushangaa yaliyokuwa yakitokea.

Balaa lilivyoanza
Akitumia Kanuni ya 69(1), Mbunge wa Mkoani (CUF), Ali Hamisi Seif, alitaka kuahirishwa kwa mjadala wa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013 kutokana na ukweli kuwa Kamati ya Sheria, Katiba na Utawala ya Bunge ilipaswa kukusanya maoni ya wadau mbalimbali nchini ikiwamo upande wa Zanzibar jambo ambalo halikufanyika wakati wa maandalizi ya muswada huo.

“Ilipaswa sheria hii inapotaka kufanyiwa marekebisho iende tena kulekule Zanzibar lakini jambo la kusikitisha kamati inayohusika na masuala ya Katiba haikwenda. Mimi ni mjumbe wa kamati na tuliitwa Dar lakini ratiba waliyotupa haikuonyesha kama tungekwenda Zanzibar,” alisema. 

Mkosamali naye aliomba mwongozo kwa Spika, akisema kwa kuzingatia matakwa ya kiapo cha Spika au Naibu alipaswa kuendesha Bunge kwa haki bila upendeleo.

“Kanuni inasema Spika ama Naibu Spika ama Mwenyekiti ataendesha shughuli za Bunge kwa haki, uadilifu, bila chuki wala upendeleo wowote kwa kuongozwa na Katiba ya nchi,” alisema na kuongeza: “Kwa kuwa sisi tumekuweka hapo ili uendeshe Bunge kwa uadilifu, usiburuzwe na chama chako na uzingatie miongozo yote kwa wakati. Kwa nini usitumie mamlaka yako kuondoa muswada huu”?

Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenister Mhagama aliomba mwongozo kwamba kwa kuwa bado kuna malalamiko basi waipe Serikali nafasi ya kuthibitisha kwamba majadiliano ya kamati yalikamilika.

Lissu katika kuomba mwongozo wake, alisema Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Sheria, Katiba na Utawala, Pindi Chana alilidanganya Bunge alipowasilisha maoni ya kamati kwamba wadau wa muswada huo walishirikishwa jambo ambalo alisema si kweli.

Lissu alisema hakuna Mzanzibari aliyefika mbele ya kamati hiyo kutoa maoni kuhusu muswada wowote.

Hata hivyo, Chana alijibu akisema wadau wa Zanzibar walitoa maoni yao na kukabidhi nyaraka mbalimbali kwa Spika kuthibitisha kauli yake hiyo. Alivitaja vyama vya Jahazi Asilia na ADC kuwa vilihojiwa.

Kwa upande wake, Lukuvi alimshambulia Lissu kwa kauli yake ya juzi kwamba uteuzi wa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanywa na Rais Jakaya Kikwete ulikuwa na walakini. “Lissu alisema jana (juzi) kwamba wapo wadau ambao walisema ijapokuwa waliandikiwa barua ya kuwasilisha majina matatu kila moja ili Rais ateue mmoja lakini hakuna mjumbe aliyeteuliwa”.

Alitaja majina ya walioteuliwa kuwa ni Maria Kashonda (Tec), Jesca Mkuchu (CCT), Humphrey Polepole (Civil Society) na Profesa Palamagamba Kabudi (Kundi la Wasomi).

Lukuvi aliwataja wengine waliopendekezwa na taasisi zao na Rais kuwateua kuwa ni Mwamtumu Malale (Bakwata) na Dk Sengondo Mvungi (NCCR) na Profesa Mwesiga Baregu wa Chadema.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Fredrick Werema alisema katika mchakato wa muswada huo, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) iliwasilisha maoni yake mbele ya kamati.

Alisema Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi aliwasilisha kwa kamati mapendekezo ya SMZ, Mei mwaka huu na mapendekezo hayo ikiwamo uteuzi wa wajumbe 166 yalizingatiwa.


Waacha muswada, wapiga vijembe
Baada ya kurejea katika kikao cha Bunge cha jioni jana, wabunge wa CCM waliopewa fursa ya kuchangia mjadala wa muswada huo walitumia muda mwingi kuwajadili wabunge wa kambi ya upinzani.